| has gloss | swa: Nonini (amezaliwa 1 Oktoba, 1982) jina lake haswa ni Hubert Nakitare, ni msanii wa nyimbo aina ya hip hop kutoka nchini kenya awali akisajiliwa na calif records,lakini baadaye alijiunga na homeboyz productions. Yeye alijitosa kwenye ulingo wa muziki wa mijini nchini Kenya kupitia wimbo wake "Nonini ni Nani?" kupanda kwa umaarufu wake kitaifa na kikanda haukuanza hata hivyo mpaka alipotowa wimbo wake "Manzi wa Nairobi" mwaka 2002, wimbo ambao ulisifu uzuri wa wanawake wa Kenya na kufuatiliwa na wimbo "Weh Kamu". Yeye aliendelia kwa kutoa albamu yake "Hanyaring game" mwishoni mwa mwaka wa 2004 ambayo ilihusisha wimbo maarufu "Keroro" neno la kisheng lenye maana ya pombe ya bia.Nonini anajulikana kwa kutoa wimbo wa kwanza wa Genge mapema katika kazi yake ya uimbaji. |